Halloween Costume ideas 2015
Latest Post

Mashabiki wengi  wa soka wanaamini nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo ndiye bora duniani..lakini kuna hili gazeti moja kutoka Ufaransa la L’Equipe limeorodhesha wachezaji 100 waliofanya vizuri kwa mwaka uliopita wa 2015.
Katika orodha hiyo Ronaldo pamoja na mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski wamefanikiwa kuingia hatua ya tano bora.
Mastaa waliofanikiwa kushika nafasi tatu za juu ni Lionel Mess, Neymar pamoja na Luis Suarez.

Pathankot
Maofisa wa polisi wakiweka doria nje ya kambi hiyo baada ya  uvamizi.



Washambuliaji wanne wameuawa baada ya wanajeshi wa India kuzima shambulio la mapema asubuhi katika kambi la jeshi la wanahewa karibu na mpaka wake na Pakistan.
Wanajeshi wawili wa kambi hiyo ya Pathankot pia waliuawa kwenye makabiliano na wapiganaji hao, ambayo yalidumu saa kadha.

Kambi hiyo imo kwenye barabara kuu ya kuelekea sehemu ya Kashmir inayodhibitiwa na Kashmir.
Shambulio hilo limetokea siku chache baada ya viongozi wa India na Pakistan Narendra Modi na Nawaz Sharif kukutana mjini Lahore kuzindua mpango wa ghafla wa kutafuta Amani.
Jimbo lote la Punjab nchini India limewekwa katika hali la tahadhari.
Watu hao walioshambulia kambi hiyo wanadaiwa kuvalia sare za jeshi la India na walitumia gari walilokuwa wameteka nyara.

Waliingia maeneo ya makazi ya wanajeshi kambini lakini wakakabiliwa vikali na hawakuweza kuharibu vifaa vya jeshi, msemaji wa jeshi la wanahewa Rochelle D'Silva amesema.
Mwandishi wa BBC Sanjoy Majumder akiwa Delhi anasema bado haijabainika washambuliaji hao walikuwa kina nani lakini wanashukiwa kutoka kundi la wapiganaji wa Kashmir kutoka upande unaodhibitiwa na Pakistan.

Hata hivyo, shirika la habari la AFP limemnukuu afisa mmoja wa usalama akisema wanaaminika kuwa wa kutoka kundi la Jaish-e-Mohammed.

India inamini kundi hilo husaidiwa na Pakistan, madai ambayo taifa hilo limekanusha.
Mwezi Agosti, watu saba waliuawa katika shambulio sawa, watu wenye silaha waliposhambulia kituo cha polisi wilaya ya Gurdaspur.

Jumapili
Majeshi ya serikali yalipoukomboa mji wa Ramad siku ya jumapili



Wapiganaji wa kundi la Islamic State (IS) wameshambulia kambi ya jeshi karibu na mji wa Ramadi, siku chache baada ya mji huo kukombolewa na wanajeshi wa serikali.

Msemaji wa jeshi amesema washambuliaji waliokuwa kwenye ndege lililotegwa mabomu na wengine waliovalia mikanda ya kujilipua walishiriki shambulio hilo.

Jeshi lilikabiliana nao likisaidiwa kutoka angani na majeshi ya muungano unaoongozwa na Marekani.
Serikali ya Iraq ilitangaza kwamba ilikuwa imefanikiwa kuukomboa mji wa Ramadi kutoka kwa IS Jumapili.

Wapiganaji hao walikuwa wameushikilia mji huo mkubwa tangu Mei.
Shambulio la Ijumaa ndilo la karibuni zaidi kutekelezwa na IS dhidi ya wanajeshi wa Iraq tangu kukombolewa kwa Ramadi.
Mtathmini wa BBC anayeangazia masuala ya Mashariki ya Kati Sebastian Usher, anasema shambulio hilo linaonyesha kibarua ambacho majeshi ya serikali yanakabiliwa nacho kulinda mji wa Ramadi.

 Kiwanda

Waislamu 200 wanaofanya kazi katika kiwanda kimoja cha nyama Colorado, Marekani wamefutwa kazi baada yao kugoma...,

 

Walikuwa wamegoma kulalamikia kunyimwa uhuru wa kuswali wakiwa kazini.
Wengi wao ni wahamiaji kutoka Somalia.
Msemaji wa Baraza la Uhusiano wa Wamarekani na Waislamu Jaylani Hussein anasema wafanyakazi hao katika kiwanda cha Cargill Meat Solutions walikuwa kwa muda mrefu wameruhusiwa kuswali.
Msemaji wa kiwanda hicho cha Cargill alisema kuna uhuru wa kuabudu kiwandani lakini lazima mahitaji ya kuabudu yaambatane na mahitaji ya kazi kiwandani.

Mkurugenzi mkuu wa Tume ya Haki za Kibinadamu Somalia Omar Jamal, amesema mameneja wanafaa kufahamu kwamba Waislamu huhitajika kuswali mara kadha kwa siku, hili likitegemea kipindi cha mwaka.

 


 
Familia nchini Uchina sasa zimeruhusiwa kupata watoto wawili baada ya kuanza kutekelezwa kwa sera mpya kuhusu upangaji uzazi.

Sera hiyo mpya imeanza kutekelezwa Ijumaa na kufikisha kikomo sera tata ya awali ambayo iliwaruhusu wanandoa kupata mtoto mmoja pekee.
Sera hiyo imesababisha kuwepo kwa sehemu kubwa ya raia ambao ni wazee na kupungua kwa watu ambao wanaweza kufanya kazi.

Sera hiyo ya watoto waili ilitangazwa Oktoba na chama tawala cha Kikomunisti na kuidhinishwa na bunge la taifa baadaye Desemba.

"Ni vyema kuzingatia jinsi maisha yataathirika,” shirika la habari la serikali la Xinhua limesema.
Sera ya kuruhusu mtoto mmoja pekee katika familia ilianza kutekelezwa mwaka 1978
Waliopata watoto zaidi waliadhibiwa vikali na hata wengine kulazimishwa kutoa mimba.
Sera hiyo ilizuia kuzaliwa kwa watu 400 milioni.
Wanandoa waliojifungua mtoto zaidi ya mmoja waliadhibiwa

Idadi ya watu Uchina kufikia 2013 wakati wa kufanywa kwa sensa ilikuwa imefikia 1.357 bilioni.
Kufikia 2050, Uchina inatarajiwa kuwa na watu karibu 500 milioni waliozidi umri wa miaka 60, idadi inayozidi raia wa Marekani.

Utafiti uliofanywa majuzi unaonyesha kwamba licha ya serikali kulegeza sheria ya kujifungua watoto, hakuna msisimko miongoni mwa wanandoa 100 milioni ambao wanaweza kupata watoto wa ziada.
Hii sana inatokana na gharama ya kuwalea watoto.

 

 

Klabu za Ligi Kuu ya England zitashuka dimbani kusaka alama za kwanza Mwaka Mpya leo Jumamosi, Arsenal wakijaribu kuendeleza uongozi kileleni kwa mechi ya nyumbani dhidi ya Newcastle.

Manchester United nao watakuwa nyumbani Old Trafford kusakata gozi dhidi ya Swansea ambao kwenye mechi za hivi karibuni wamekuwa wakiwalemea.

 

Manchester City watakuwa ugenini baadaye dhidi ya Watford. 


Chelsea watasubiri hadi Jumapili kujaribu bahati watakapokuwa ugenini dhidi ya Crystal Palace.

Ratiba kamili ya mechi ni kama ifuatavyo:
Jumamosi 2 Januari 2016 (Saa za Afrika Mashariki)
  • West Ham v Liverpool 15:45
  • Arsenal v Newcastle 18:00
  • Leicester v Bournemouth 18:00
  • Man Utd v Swansea 18:00
  • Norwich v Southampton 18:00
  • Sunderland v Aston Villa 18:00
  • West Brom v Stoke 18:00
  • Watford v Man City 20:30
Jumapili 2 Januari 2016
  • Crystal Palace v Chelsea 16:30
  • Everton v Tottenham 19:00
Jumanne 2 Januari 2016
  • Aston Villa v Crystal Palace 22:45
  • Bournemouth v West Ham 22:45

 

Makabiliano makali katika mkesha wa Mwaka Mpya baina ya wafungwa katika gereza moja la mashariki mwa Guatemala yamesababisha vifo vya watu wanane na wengine 24 kujeruhiwa. Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari, wawili kati ya waliokufa walikatwakatwa na kisha miili yao ikachomwa moto...,


 

 Polisi wa kutuliza ghasia walichukua udhibiti wa gereza hilo jana Ijumaa. Maafisa waligundua kuwa wafungwa hao walijaribu kutoroka kwa kubomoa ukuta wa gereza hilo la Puerto Barrios ambalo lina msongamano mkubwa kabisa wa wafungwa.

 Limejengwa kuwa na uwezo wa kuwahifadhi wafungwa 175, lakini sasa lina wafungwa 944. Tukio hilo ni la karibuni katika msururu wa mapigano ya gerezani nchini humo katika miaka ya karibuni. Mwezi Novemba mwaka jana, wafungwa 16 waliuawa kufuatia rabsha gerezani, huku wahanga watatu wakikatwakatwa vibaya.

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget